17 Mikono yenu haipaswi kuchukua kitu chochote kinachopaswa kuharibiwa,*+ ili Yehova aache hasira yake kali na kuwaonyesha rehema na huruma na kuwafanya mwongezeke, kama alivyowaapia mababu zenu.+
11 Waisraeli wametenda dhambi. Wamevunja agano langu+ nililowaamuru washike. Wamechukua baadhi ya vitu vilivyopaswa kuharibiwa,+ wameviiba+ na kuvificha kati ya vitu vyao.+
21 Nilipoona katika nyara vazi rasmi maridadi kutoka Shinari+ na shekeli 200 za fedha na kipande kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 50,* nilivitamani, kwa hiyo nikavichukua. Nimevificha ardhini ndani ya hema langu, na fedha ziko chini yake.”