10 Basi wakalipeleka Sanduku la Mungu wa kweli kule Ekroni,+ lakini mara tu Sanduku la Mungu wa kweli lilipofika Ekroni, Waekroni wakaanza kulia kwa sauti wakisema: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli ili watuue sisi pamoja na watu wetu!”+
14 Pia, majiji ambayo Wafilisti walikuwa wamechukua kutoka kwa Waisraeli yalirudishwa kwa Waisraeli, kuanzia Ekroni mpaka Gathi, na Waisraeli wakayakomboa maeneo yao kutoka mikononi mwa Wafilisti.
Pia kukawa na amani kati ya Waisraeli na Waamori.+
2 Huo ndio wakati ambapo Ahazia alianguka chini kupitia kiunzi kilichokuwa katika chumba chake cha darini kule Samaria, akajeruhiwa. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Nendeni mkamuulize Baal-zebubu mungu wa Ekroni+ ikiwa nitapona jeraha hili.”+