20 Basi watu wakapaza sauti pembe zilipopigwa.+ Na mara tu watu waliposikia sauti za pembe na kupiga kelele kubwa za vita, ukuta ukaanguka chini.+ Kisha kila mtu akaingia jijini moja kwa moja, nao wakaliteka.
26 Wakati huo Yoshua alitangaza kiapo* hiki: “Na alaaniwe mbele za Yehova mtu atakayejaribu kulijenga tena jiji hili la Yeriko. Atakapojenga msingi wake, mzaliwa wake wa kwanza atakufa, na atakapoweka malango yake, mwana wake wa mwisho atakufa.”+