Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 1:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Mwaka baada ya mwaka mwanamume huyo alitoka katika jiji lake na kupanda kwenda Shilo kumwabudu* na kumtolea dhabihu Yehova wa majeshi.+ Wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi,+ walitumikia huko wakiwa makuhani wa Yehova.+

  • 1 Samweli 4:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Watu waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakasema hivi: “Kwa nini Yehova ameruhusu tushindwe leo na Wafilisti?*+ Na tujichukulie sanduku la agano la Yehova kutoka Shilo,+ twende nalo ili lituokoe kutoka mikononi mwa maadui wetu.”

  • Zaburi 78:60
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 60 Mwishowe akaliacha hema la ibada lililo Shilo,+

      Hema alimokaa miongoni mwa wanadamu.+

  • Yeremia 7:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “‘Hata hivyo, sasa nendeni mahali pangu huko Shilo,+ ambapo mwanzoni nilifanya jina langu likae,+ na kuona nilivyopafanya kwa sababu ya uovu wa watu wangu Waisraeli.+

  • Matendo 7:44, 45
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 “Mababu zetu walikuwa na hema la ushahidi nyikani, lililotengenezwa kwa kufuata maagizo ambayo Mungu alimpa Musa kulingana na mfano aliokuwa amemwonyesha.+ 45 Nao mababu zetu wakalimiliki na kulileta pamoja na Yoshua kwenye nchi iliyomilikiwa na mataifa,+ ambayo Mungu aliyafukuza kutoka mbele ya mababu zetu.+ Nalo likakaa huko mpaka siku za Daudi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki