-
Yoshua 10:11-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli, Yehova akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka angani kwenye mteremko wa Beth-horoni mpaka Azeka, nao wakafa. Kwa kweli, wale waliouawa na mvua ya mawe walikuwa wengi kuliko wale waliouawa na Waisraeli kwa upanga.
12 Ni siku hiyo, siku ambayo Yehova aliwashinda kabisa Waamori mbele ya Waisraeli, ndipo Yoshua alipomwambia hivi Yehova mbele ya Waisraeli:
13 Basi jua likasimama tuli na mwezi ukatulia mpaka taifa la Israeli lilipolipiza kisasi dhidi ya maadui wake. Je, haijaandikwa hivi katika kitabu cha Yashari:+ Jua lilisimama tuli katikati ya mbingu na halikutua kwa siku nzima? 14 Haijawahi kamwe kutokea siku kama hiyo, kabla au baada yake, ambayo Yehova aliisikiliza sauti ya mwanadamu+ katika njia hiyo, kwa sababu Yehova alikuwa akiwapigania Waisraeli.+
-