-
Hesabu 11:16, 17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Yehova akamjibu Musa: “Nikusanyie wanaume 70 miongoni mwa wazee wa Israeli, wanaume ambao unajua kwamba ni wazee na maofisa wa watu,+ nawe uwapeleke kwenye hema la mkutano, na kuwaagiza wasimame hapo pamoja nawe. 17 Nitashuka+ na kuzungumza nawe hapo,+ nami nitachukua kiasi fulani cha roho+ iliyo juu yako na kuiweka juu yao, nao watakusaidia kubeba mzigo wa watu hawa ili usiubebe peke yako.+
-
-
Waamuzi 14:5, 6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Basi Samsoni akaenda na baba yake na mama yake hadi Timna. Alipofika katika mashamba ya mizabibu ya Timna, simba* akamjia akinguruma. 6 Ndipo roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ naye akampasua simba huyo vipande viwili, kama mtu anavyompasua mwanambuzi kwa mikono yake. Lakini hakumwambia baba yake au mama yake jambo alilofanya.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 15:1Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Sasa roho ya Mungu ilimjia Azaria mwana wa Odedi.
-