Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 11:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Yehova akamjibu Musa: “Nikusanyie wanaume 70 miongoni mwa wazee wa Israeli, wanaume ambao unajua kwamba ni wazee na maofisa wa watu,+ nawe uwapeleke kwenye hema la mkutano, na kuwaagiza wasimame hapo pamoja nawe. 17 Nitashuka+ na kuzungumza nawe hapo,+ nami nitachukua kiasi fulani cha roho+ iliyo juu yako na kuiweka juu yao, nao watakusaidia kubeba mzigo wa watu hawa ili usiubebe peke yako.+

  • Waamuzi 6:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Kisha roho ya Yehova ikamjia* Gideoni+ naye akapiga pembe,*+ na Waabiezeri+ wakakusanyika na kumfuata.

  • Waamuzi 11:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Roho ya Yehova ikamjia Yeftha,+ naye akapitia Gileadi na Manase na kufika Mispe kule Gileadi,+ na kutoka Mispe akaenda kupigana na Waamoni.

  • Waamuzi 14:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Basi Samsoni akaenda na baba yake na mama yake hadi Timna. Alipofika katika mashamba ya mizabibu ya Timna, simba* akamjia akinguruma. 6 Ndipo roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ naye akampasua simba huyo vipande viwili, kama mtu anavyompasua mwanambuzi kwa mikono yake. Lakini hakumwambia baba yake au mama yake jambo alilofanya.

  • Waamuzi 15:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Alipofika Lehi, Wafilisti walishangilia sana kumwona. Kisha roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ na kamba alizofungwa mikononi zikawa kama nyuzi za kitani zilizochomwa moto, nazo zikalegea* na kuanguka kutoka mikononi mwake.+

  • 1 Samweli 11:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Roho ya Mungu ikamtia nguvu Sauli+ alipoyasikia maneno hayo, akawaka hasira.

  • 1 Samweli 16:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Basi Samweli akachukua ile pembe ya mafuta+ na kumtia mafuta mbele ya ndugu zake. Na roho ya Yehova ikaanza kumtia nguvu Daudi kuanzia siku hiyo na kuendelea.+ Baadaye Samweli akainuka na kwenda zake Rama.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 15:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Sasa roho ya Mungu ilimjia Azaria mwana wa Odedi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki