Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 3:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Waisraeli walipomlilia Yehova awasaidie,+ Yehova aliwapa mwokozi ili awaokoe,+ Othnieli+ mwana wa Kenasi, ndugu mdogo wa Kalebu. 10 Roho ya Yehova ikamjia,+ akawa mwamuzi wa Israeli. Alipoenda vitani, Yehova alimtia Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia* mikononi mwake, naye akamshinda Kushan-rishathaimu.

  • Waamuzi 6:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Kisha roho ya Yehova ikamjia* Gideoni+ naye akapiga pembe,*+ na Waabiezeri+ wakakusanyika na kumfuata.

  • Waamuzi 11:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Roho ya Yehova ikamjia Yeftha,+ naye akapitia Gileadi na Manase na kufika Mispe kule Gileadi,+ na kutoka Mispe akaenda kupigana na Waamoni.

  • Waamuzi 14:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Basi Samsoni akaenda na baba yake na mama yake hadi Timna. Alipofika katika mashamba ya mizabibu ya Timna, simba* akamjia akinguruma. 6 Ndipo roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ naye akampasua simba huyo vipande viwili, kama mtu anavyompasua mwanambuzi kwa mikono yake. Lakini hakumwambia baba yake au mama yake jambo alilofanya.

  • 1 Samweli 10:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Basi wakatoka hapo na kupanda kwenye kilima, na kikundi cha manabii kikakutana naye. Mara moja roho ya Mungu ikamtia nguvu,+ naye akaanza kutoa unabii+ kati yao. 11 Watu wote waliomjua awali walipomwona akitoa unabii pamoja na manabii, wakaulizana: “Mwana wa Kishi amepatwa na nini? Je, Sauli pia ni mmoja wa manabii?”

  • 1 Samweli 16:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Basi Samweli akachukua ile pembe ya mafuta+ na kumtia mafuta mbele ya ndugu zake. Na roho ya Yehova ikaanza kumtia nguvu Daudi kuanzia siku hiyo na kuendelea.+ Baadaye Samweli akainuka na kwenda zake Rama.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki