-
Yoshua 15:16-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Ndipo Kalebu akasema: “Yeyote atakayeshambulia na kuteka jiji la Kiriath-seferi, nitampa binti yangu Aksa awe mke wake.” 17 Othnieli+ mwana wa Kenasi,+ ndugu ya Kalebu, akaliteka. Kwa hiyo akampa Aksa+ binti yake awe mke wake. 18 Mwanamke huyo alipokuwa akienda nyumbani kwake, akamsihi mume wake amwombe baba* yake shamba. Kisha mwanamke huyo akashuka kutoka juu ya punda wake.* Kalebu akamuuliza: “Unataka nini?”+ 19 Akamwambia: “Tafadhali nibariki, kwa maana umenipa shamba upande wa kusini;* nipe pia Guloth-maimu.”* Basi Kalebu akampa Gulothi ya Juu na Gulothi ya Chini.
-