-
Hesabu 10:29-32Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Kisha Musa akamwambia Hobabu mwana wa Reueli,*+ Mmidiani, baba mkwe wake: “Tunaenda mahali ambapo Yehova alisema, ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’+ Basi twende pamoja,+ nasi tutakutendea mema, kwa sababu Yehova ameahidi kuwapa Waisraeli mambo mema.”+ 30 Lakini akamwambia: “Sitaenda. Nitarudi katika nchi yangu na kwa watu wangu wa ukoo.” 31 Musa akamwambia: “Tafadhali usituache, kwa maana unajua mahali tunapopaswa kupiga kambi nyikani, nawe unaweza kutuonyesha njia.* 32 Ukienda pamoja nasi,+ jambo lolote jema ambalo Yehova atatutendea, bila shaka tutakutendea wewe pia.”
-