16 Na wazao wa Mkeni,+ baba mkwe wa Musa,+ walitoka katika lile jiji la mitende+ pamoja na watu wa Yuda na kwenda katika nyika ya Yuda, upande wa kusini wa Aradi.+ Wakakaa huko pamoja na wenyeji.+
11 Lakini Heberi Mkeni alikuwa amejitenga na Wakeni,+ waliokuwa wazao wa Hobabu, baba mkwe wa Musa,+ naye alipiga hema lake karibu na mti mkubwa uliokuwa Saananimu, kule Kedeshi.
6 Ndipo Sauli akawaambia hivi Wakeni:+ “Nendeni, ondokeni kati ya Waamaleki ili nisiwafagilie mbali pamoja nao.+ Kwa maana mliwatendea watu wote wa Israeli+ kwa upendo mshikamanifu walipotoka Misri.” Basi Wakeni wakaondoka kati ya Waamaleki.