3Musa akawa mchungaji wa kondoo wa Yethro,+ baba mkwe wake, kuhani wa Midiani. Alipokuwa akiwaongoza kondoo kuelekea upande wa magharibi wa nyika, hatimaye alifika kwenye mlima wa Mungu wa kweli ulioitwa Horebu.+
18 Basi Musa akarudi kwa Yethro baba mkwe wake+ na kumwambia: “Ninataka kwenda, tafadhali, nirudi kwa ndugu zangu walio Misri nione kama wangali hai.” Yethro akamwambia Musa: “Nenda kwa amani.”
18Sasa Yethro kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Musa,+ akasikia mambo yote ambayo Mungu alikuwa amemtendea Musa na watu wake Waisraeli, jinsi Yehova alivyowatoa Waisraeli nchini Misri.+
29 Kisha Musa akamwambia Hobabu mwana wa Reueli,*+ Mmidiani, baba mkwe wake: “Tunaenda mahali ambapo Yehova alisema, ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’+ Basi twende pamoja,+ nasi tutakutendea mema, kwa sababu Yehova ameahidi kuwapa Waisraeli mambo mema.”+