-
Kumbukumbu la Torati 13:5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Lakini nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto anapaswa kuuawa,+ kwa sababu aliwachochea mmwasi Yehova Mungu wenu—aliyewatoa nchini Misri na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa—ili mtoke katika njia ambayo Yehova Mungu wenu amewaamuru mtembee. Nanyi lazima mwondoe kilicho kiovu kutoka miongoni mwenu.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 17:2-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 “Ikiwa mwanamume au mwanamke atapatikana miongoni mwenu, katika mojawapo ya majiji ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, aliye na mazoea ya kufanya uovu machoni pa Yehova Mungu wenu na kuvunja agano lake,+ 3 naye anapotoka na kuabudu miungu mingine na kuiinamia miungu hiyo au jua au mwezi au jeshi lote la mbinguni,+ jambo ambalo sijaamuru,+ 4 ukiambiwa au kusikia habari hiyo, unapaswa kuchunguza jambo hilo kikamili. Ikithibitishwa ni kweli+ kwamba jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa katika Israeli, 5 utamtoa nje ya malango ya jiji lenu mwanamume au mwanamke ambaye amefanya uovu huo, na lazima mwanamume au mwanamke huyo auawe kwa kupigwa mawe.+
-