24 Baadaye mwanamke huyo akazaa mwana na kumpa jina Samsoni;+ na mvulana huyo akazidi kukua, na Yehova akaendelea kumbariki. 25 Baada ya muda roho ya Yehova ikaanza kumchochea+ huko Mahane-dani+ kati ya Sora na Eshtaoli.+
6 Ndipo roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ naye akampasua simba huyo vipande viwili, kama mtu anavyompasua mwanambuzi kwa mikono yake. Lakini hakumwambia baba yake au mama yake jambo alilofanya.
14 Alipofika Lehi, Wafilisti walishangilia sana kumwona. Kisha roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ na kamba alizofungwa mikononi zikawa kama nyuzi za kitani zilizochomwa moto, nazo zikalegea* na kuanguka kutoka mikononi mwake.+