-
Waamuzi 2:20-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Mwishowe hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli,+ akasema, “Kwa sababu taifa hili limevunja agano langu+ nililofanya na mababu zao, na halijanitii,+ 21 basi mimi sitafukuza kutoka mbele yao taifa hata moja ambalo Yoshua aliacha alipokufa.+ 22 Nitafanya hivyo ili kuwajaribu Waisraeli nione kama wataishika njia yangu mimi, Yehova,+ na kutembea katika njia hiyo kama baba zao walivyofanya.” 23 Kwa hiyo Yehova akaruhusu mataifa hayo yabaki. Hakuyafukuza haraka, wala hakuyatia mikononi mwa Yoshua.
-