3 Kisha Musa akaja na kuwaambia watu maneno yote ya Yehova na sheria zote,*+ na watu wote wakajibu hivi kwa sauti moja: “Maneno yote ambayo Yehova amesema, tuko tayari kuyafanya.”+
8 Basi Musa akachukua damu akawanyunyizia watu+ na kusema: “Hii ndiyo damu ya agano ambalo Yehova amefanya pamoja nanyi kulingana na maneno hayo yote.”+
27 Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Unapaswa kuandika maneno haya,+ kwa sababu kulingana na maneno haya, ninafanya agano pamoja nawe na pamoja na Israeli.”+
29Haya ndiyo maneno ya agano ambalo Yehova alimwamuru Musa afanye pamoja na Waisraeli katika nchi ya Moabu, mbali na agano alilofanya nao kule Horebu.+
16 Mkivunja agano la Yehova Mungu wenu alilowaamuru mshike na mkienda kuabudu miungu mingine na kuiinamia, hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu+ nanyi mtaangamia haraka kutoka katika nchi nzuri ambayo amewapa.”+