4 Basi wakauliza: “Tunapaswa kumpelekea dhabihu gani ya hatia?” Wakasema: “Kulingana na idadi ya watawala wa Wafilisti,+ pelekeni bawasiri tano za dhahabu na panya watano wa dhahabu, kwa maana kila mmoja wenu pamoja na watawala wenu wamepatwa na pigo lilelile.
17 Basi hizi ndizo bawasiri za dhahabu ambazo Wafilisti walimletea Yehova kuwa dhabihu ya hatia:+ moja kwa ajili ya Ashdodi,+ moja kwa ajili ya Gaza, moja kwa ajili ya Ashkeloni, moja kwa ajili ya Gathi,+ moja kwa ajili ya Ekroni.+