-
1 Samweli 6:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Wakajibu: “Mkilirudisha sanduku la agano la Yehova, Mungu wa Israeli, msilirudishe bila dhabihu. Kwa vyovyote vile mnapaswa kumrudishia pamoja na dhabihu ya hatia.+ Ndipo tu mtakapoponywa, nanyi mtajulishwa kwa nini mkono wake unaendelea kuwaadhibu.” 4 Basi wakauliza: “Tunapaswa kumpelekea dhabihu gani ya hatia?” Wakasema: “Kulingana na idadi ya watawala wa Wafilisti,+ pelekeni bawasiri tano za dhahabu na panya watano wa dhahabu, kwa maana kila mmoja wenu pamoja na watawala wenu wamepatwa na pigo lilelile.
-