-
Yoshua 7:16-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Kesho yake, Yoshua akaamka asubuhi na mapema akawakusanya Waisraeli, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda likachaguliwa. 17 Kisha akaleta karibu koo za Yuda na ukoo wa Wazera+ ukachaguliwa, kisha akaleta karibu familia za ukoo wa Wazera, mwanamume kwa mwanamume, na Zabdi akachaguliwa. 18 Mwishowe akaleta karibu familia ya Zabdi, mwanamume kwa mwanamume, naye Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, akachaguliwa.+
-