-
1 Samweli 21:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Baadaye Daudi akafika Nobu+ kwa kuhani Ahimeleki. Ahimeleki alianza kutetemeka alipokutana na Daudi, akamuuliza: “Kwa nini uko peke yako na hujaja na mtu yeyote?”+ 2 Daudi akamjibu kuhani Ahimeleki: “Mfalme aliniagiza nifanye jambo fulani, lakini akaniambia, ‘Usimjulishe mtu yeyote kazi niliyokutuma kufanya na maagizo niliyokupa.’ Nilikubaliana na vijana wangu tukutane mahali fulani.
-