Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 28:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Wafilisti wakakusanyika na kwenda kupiga kambi Shunemu.+ Basi Sauli akawakusanya Waisraeli wote, nao wakapiga kambi Gilboa.+

  • 2 Samweli 1:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Enyi milima ya Gilboa,+

      Msipate umande wowote wala mvua yoyote,

      Wala mashamba yanayozaa michango mitakatifu,+

      Kwa sababu ngao ya wenye nguvu ilichafuliwa huko,

      Sasa ngao ya Sauli haijatiwa mafuta.

  • 1 Mambo ya Nyakati 10:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Sasa Wafilisti walikuwa wakipigana na Waisraeli. Na wanaume wa Israeli wakawakimbia Wafilisti, na wengi wakauawa kwenye Mlima Gilboa.+ 2 Wafilisti wakamkaribia sana Sauli na wanawe, nao wakamuua Yonathani, Abinadabu, na Malki-shua,+ wana wa Sauli. 3 Vita vikawa vikali sana dhidi ya Sauli, na wapiga mishale wakampata na kumjeruhi.+ 4 Ndipo Sauli akamwambia mtu aliyembebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa wasije kunitendea kikatili.”*+ Lakini mtu aliyembebea silaha hakutaka kufanya hivyo, kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga na kuuangukia.+ 5 Mtu aliyembebea silaha alipoona kwamba Sauli amekufa, yeye pia akauangukia upanga wake mwenyewe na kufa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki