-
1 Mambo ya Nyakati 14:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Mfalme Hiramu+ wa Tiro aliwatuma wajumbe kwa Daudi, pamoja na mbao za mierezi, waashi,* na maseremala ili wamjengee Daudi nyumba.*+ 2 Na Daudi alijua kwamba Yehova alikuwa amemwimarisha kabisa kuwa mfalme wa Israeli,+ kwa maana ufalme wake ulikuwa umekwezwa sana kwa ajili ya watu Wake Waisraeli.+
-