Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 13:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Ndipo Samweli akamwambia Sauli: “Umetenda kipumbavu. Hukutii amri ambayo Yehova Mungu wako alikupa.+ Kama ungetii, Yehova angeimarisha ufalme wako juu ya Waisraeli milele. 14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu.+ Yehova atamtafuta mtu anayeupendeza moyo wake,+ na Yehova atamweka kuwa kiongozi juu ya watu wake,+ kwa sababu hukutii mambo uliyoamriwa na Yehova.”+

  • 1 Samweli 15:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Samweli alipokuwa akigeuka aende zake, Sauli akaushika upindo wa joho lake lisilo na mikono, lakini likararuka. 28 Ndipo Samweli akamwambia: “Yehova ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako leo, naye atampa mwenzako aliye bora kuliko wewe.+

  • 1 Samweli 16:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Mwishowe Yehova akamuuliza Samweli: “Kwa kuwa nimemkataa Sauli asitawale akiwa mfalme wa Israeli,+ utaendelea kumwombolezea mpaka lini?+ Jaza pembe yako mafuta,+ uende. Nitakutuma kwa Yese+ Mbethlehemu, kwa sababu nimejichagulia mfalme kutoka miongoni mwa wanawe.”+

  • 1 Samweli 16:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Basi akamtuma mtu amwite, Yese akamleta ndani. Kijana huyo alikuwa mwekundu, mwenye macho yanayovutia, na mwenye sura nzuri.+ Ndipo Yehova akasema: “Simama, mtie mafuta, kwa maana huyu ndiye!”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki