-
1 Mambo ya Nyakati 17:23-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Sasa, Ee Yehova, ahadi uliyotoa kunihusu mimi mtumishi wako na nyumba yangu na ithibitike kuwa ya uaminifu milele, na ufanye kama ulivyoahidi.+ 24 Jina lako na lidumu na kukwezwa+ milele, ili watu waseme, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, ni Mungu kwa Israeli,’ na nyumba yangu mimi mtumishi wako Daudi na iimarishwe kabisa mbele zako.+ 25 Kwa maana wewe, Mungu wangu, umenifunulia mimi mtumishi wako kusudi lako la kunijengea nyumba.* Ndiyo sababu mimi mtumishi wako nina ujasiri wa kutoa sala hii kwako. 26 Na sasa, Ee Yehova, wewe ndiye Mungu wa kweli, nawe umeahidi mambo hayo mema kunihusu mimi mtumishi wako. 27 Basi na ufurahie kuibariki nyumba yangu mimi mtumishi wako, na idumu milele mbele zako, kwa sababu wewe, Ee Yehova, umeibariki, nayo imebarikiwa milele.”
-