-
1 Mambo ya Nyakati 19:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Daudi alipoambiwa habari hiyo, akawakusanya Waisraeli wote mara moja, wakavuka Yordani na kuwafikia, wakajipanga kivita ili kupigana nao. Daudi alijipanga kivita ili kupigana na Wasiria, nao wakapigana naye.+ 18 Lakini Wasiria waliwakimbia Waisraeli; Daudi akawaua Wasiria 7,000 walioendesha magari ya vita na wanajeshi 40,000 waliotembea kwa miguu, akamuua Shofaki mkuu wa jeshi. 19 Watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli,+ mara moja wakafanya amani na Daudi, wakawa watumishi wake;+ na Wasiria hawakutaka kuwasaidia tena Waamoni.
-