-
2 Samweli 10:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Daudi alipoambiwa habari hiyo, akawakusanya mara moja Waisraeli wote, wakavuka Yordani na kufika Helamu. Kisha Wasiria wakajipanga kivita ili kwenda kupigana na Daudi.+ 18 Lakini Wasiria wakawakimbia Waisraeli; na Daudi akawaua Wasiria 700 wanaoendesha magari ya vita na wapanda farasi 40,000, naye akampiga Shobaki mkuu wa jeshi, akafa huko.+ 19 Wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, mara moja wakafanya amani na Waisraeli, wakawa watumishi wao;+ na Wasiria wakaogopa kuwasaidia tena Waamoni.
-