Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 1:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Wakunga hao wakamjibu Farao: “Wanawake Waebrania si kama wanawake Wamisri. Wana nguvu nao huzaa kabla mkunga hajafika.”

  • Yoshua 2:3-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Ndipo mfalme wa Yeriko akawatuma wajumbe kwa Rahabu, akisema: “Watoe nje wanaume waliokuja nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi nzima.”

      4 Lakini mwanamke huyo alikuwa amewaficha wanaume hao wawili. Basi akasema: “Ni kweli, wanaume hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka. 5 Giza lilipoingia, waliondoka kabla ya lango la jiji kufungwa. Sijui walikokwenda, mkiwafuatia haraka, mtawafikia.”

  • 1 Samweli 19:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Mara moja Mikali akamteremsha Daudi kupitia dirishani, ili akimbie na kutoroka.

  • 1 Samweli 19:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Basi Sauli akawatuma wajumbe wamlete Daudi, lakini mke wa Daudi akawaambia: “Ni mgonjwa.”

  • 1 Samweli 21:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Daudi akamjibu kuhani Ahimeleki: “Mfalme aliniagiza nifanye jambo fulani, lakini akaniambia, ‘Usimjulishe mtu yeyote kazi niliyokutuma kufanya na maagizo niliyokupa.’ Nilikubaliana na vijana wangu tukutane mahali fulani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki