-
2 Samweli 3:2-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Wakati huo, Daudi akazaa wana huko Hebroni.+ Mzaliwa wake wa kwanza aliitwa Amnoni+ na mama yake alikuwa Ahinoamu+ wa Yezreeli. 3 Mzaliwa wake wa pili alikuwa Kileabu na mama yake alikuwa Abigaili,+ mjane wa Nabali Mkarmeli; na wa tatu alikuwa Absalomu+ mwana wa Maaka, binti ya Talmai+ mfalme wa Geshuri. 4 Wa nne alikuwa Adoniya+ mwana wa Hagithi, na wa tano alikuwa Shefatia mwana wa Abitali. 5 Wa sita alikuwa Ithreamu mwana wa Egla, mke wa Daudi. Hao ndio wana ambao Daudi aliwazaa huko Hebroni.
-