-
1 Mambo ya Nyakati 20:6-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Vita vikatokea tena huko Gathi,+ ambako kulikuwa na mwanamume mkubwa isivyo kawaida,+ mwenye vidole 6 katika kila mkono na vidole 6 katika kila mguu, jumla ya vidole 24; naye pia alikuwa mzao wa Warefaimu.+ 7 Aliendelea kuwadhihaki+ Waisraeli. Basi Yonathani mwana wa Shimea,+ ndugu ya Daudi, akamuua.
8 Watu hao walikuwa wazao wa Warefaimu+ huko Gathi,+ na Daudi na watumishi wake ndio waliowaua.
-