-
2 Samweli 21:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Vita vikatokea tena huko Gathi, ambako kulikuwa na mwanamume mkubwa isivyo kawaida, mwenye vidole 6 katika kila mkono na vidole 6 katika kila mguu, jumla ya vidole 24; naye pia alikuwa mzao wa Warefaimu.+ 21 Aliendelea kuwadhihaki Waisraeli.+ Basi Yonathani mwana wa Shimei,+ ndugu ya Daudi, akamuua.
22 Watu hao wanne walikuwa wazao wa Warefaimu huko Gathi, na Daudi na watumishi wake ndio waliowaua.+
-