-
1 Mambo ya Nyakati 11:12-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Aliyemfuata ni Eleazari+ mwana wa Dodo mwana wa Ahohi.+ Alikuwa miongoni mwa mashujaa hao watatu hodari. 13 Alikuwa na Daudi kule Pas-damimu,+ ambako Wafilisti walikuwa wamekusanyika kwa ajili ya vita. Basi palikuwa na shamba lililojaa shayiri, na watu walikuwa wamekimbia kwa sababu ya Wafilisti. 14 Lakini alisimama katikati ya shamba hilo na kuwazuia Wafilisti wasiingie humo, naye aliendelea kuwaua Wafilisti, hivi kwamba Yehova akawapa ushindi* mkubwa.+
-