14 Alipofika Lehi, Wafilisti walishangilia sana kumwona. Kisha roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ na kamba alizofungwa mikononi zikawa kama nyuzi za kitani zilizochomwa moto, nazo zikalegea* na kuanguka kutoka mikononi mwake.+
6 Basi Yonathani akamwambia mtumishi wake aliyembebea silaha: “Njoo tuvuke na kwenda kwenye kituo cha ulinzi cha wanaume hawa wasiotahiriwa.+ Labda Yehova atatusaidia, kwa maana hakuna kitu chochote kinachoweza kumzuia Yehova kuokoa kwa kutumia watu wengi au wachache.”+
5 Alihatarisha uhai wake* alipomuua yule Mfilisti,+ na Yehova akawapa Waisraeli wote ushindi* mkubwa. Uliona jambo hilo, ukashangilia sana. Basi kwa nini uitendee dhambi damu isiyo na hatia kwa kuagiza Daudi auawe bila sababu?”+