-
1 Mambo ya Nyakati 11:22-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Benaya+ mwana wa Yehoyada alikuwa mwanamume jasiri* aliyefanya mambo mengi ya kishujaa kule Kabzeeli.+ Aliwaua wana wawili wa Arieli wa Moabu, naye aliingia ndani ya shimo la maji siku ya theluji na kumuua simba.+ 23 Alimuua pia mwanamume Mmisri aliyekuwa mkubwa isivyo kawaida—mwenye urefu wa mikono mitano.*+ Ingawa Mmisri huyo alikuwa na mkuki mkononi kama mti wa wafumaji wa nguo,+ Benaya alikabiliana naye akiwa na fimbo, akamnyang’anya Mmisri huyo mkuki kutoka mkononi mwake na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.+ 24 Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, naye alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu hodari. 25 Ingawa alikuwa mashuhuri hata kuliko wale 30, hakuwa shujaa kama wale watatu.+ Lakini Daudi alimweka kuwa kiongozi wa walinzi wake binafsi.
-