-
1 Mambo ya Nyakati 21:8-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Basi Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Nimetenda dhambi+ kubwa kwa kufanya jambo hili. Na sasa, tafadhali, nisamehe kosa langu mimi mtumishi wako,+ kwa maana nimetenda kwa upumbavu sana.”+ 9 Kisha Yehova akamwambia hivi Gadi,+ mwonaji wa Daudi: 10 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakupa mambo matatu ya kuchagua. Chagua jambo nitakalokutendea.”’” 11 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Chagua 12 ikiwa unataka miaka mitatu ya njaa kali,+ au ikiwa unataka maadui wako wakufagilie mbali kwa miezi mitatu huku upanga wao ukikuandama,+ au siku tatu za upanga kutoka kwa Yehova—nchi ikumbwe na ugonjwa hatari+—huku malaika wa Yehova akileta maangamizi+ katika eneo lote la Israeli.’ Sasa fikiria jibu ninalopaswa kumpa Yule aliyenituma.” 13 Kwa hiyo Daudi akamwambia Gadi: “Jambo hilo linanihuzunisha sana. Tafadhali, acha nianguke mkononi mwa Yehova, kwa maana rehema zake ni nyingi sana;+ lakini usiniache nianguke mkononi mwa mwanadamu.”+
-