-
1 Mambo ya Nyakati 21:16, 17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Daudi alipoinua macho yake, alimwona malaika wa Yehova akiwa amesimama kati ya dunia na mbingu akiwa ameshika mkononi mwake upanga uliochomolewa+ na kuelekezwa Yerusalemu. Mara moja, Daudi na wazee, wakiwa wamevaa nguo za magunia,+ wakajiangusha chini kifudifudi.+ 17 Daudi akamwambia Mungu wa kweli: “Je, si mimi niliyesema watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi, na mimi ndiye niliyekosea;+ lakini kondoo hawa—wamefanya nini? Ee Yehova Mungu wangu, tafadhali, acha mkono wako uniadhibu mimi na nyumba ya baba yangu; lakini usiwapige watu wako.”+
-