-
1 Mambo ya Nyakati 21:24-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Hata hivyo, Mfalme Daudi akamwambia Ornani: “Hapana, ni lazima niununue kwa bei kamili, kwa sababu sitachukua kitu chako na kumpa Yehova au kutoa dhabihu za kuteketezwa ambazo hazinigharimu chochote.”+ 25 Basi Daudi akampimia Ornani shekeli 600 za dhahabu* kwa ajili ya uwanja huo. 26 Kisha Daudi akamjengea Yehova madhabahu+ mahali hapo na kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, akasali kwa Yehova, ambaye sasa alimjibu kwa kushusha moto+ kutoka mbinguni kwenye madhabahu hiyo ya dhabihu za kuteketezwa. 27 Kisha Yehova akamwagiza yule malaika+ aurudishe upanga wake kwenye ala. 28 Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Yehova amemjibu kwenye uwanja wa kupuria wa Ornani Myebusi, akaendelea kutoa dhabihu hapo.
-