Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 17:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 mnapaswa kumweka mfalme ambaye Yehova Mungu wenu atamchagua.+ Mnapaswa kumchagua mfalme kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Hamruhusiwi kumweka mfalme ambaye ni mgeni, ambaye si ndugu yenu. 16 Hata hivyo, hapaswi kujipatia farasi wengi+ au kuwafanya watu warudi Misri kuchukua farasi wengi zaidi,+ kwa kuwa Yehova aliwaambia hivi: ‘Msirudi huko tena kamwe kupitia njia hii.’

  • 1 Wafalme 10:24-26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Na watu wote duniani walitaka kukutana na* Sulemani ili wasikie hekima yake ambayo Mungu alikuwa ameweka moyoni mwake.+ 25 Kila mmoja wao alileta zawadi—vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, mavazi, silaha, mafuta ya zeri, farasi, na nyumbu—na walifanya hivyo mwaka baada ya mwaka.

      26 Na Sulemani akaendelea kukusanya magari ya vita na farasi;* akawa na magari 1,400 ya vita na farasi* 12,000,+ naye aliwaweka katika majiji ya magari ya vita karibu naye huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 1:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Sulemani akaendelea kukusanya magari ya vita na farasi;* akawa na magari 1,400 ya vita na farasi* 12,000,+ naye aliwaweka katika majiji ya magari ya vita+ karibu naye huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 1:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kila gari kutoka Misri lilinunuliwa kwa vipande 600 vya fedha, na farasi alinunuliwa kwa vipande 150; kisha waliwauzia wafalme wote wa Wahiti na wafalme wa Siria.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki