-
2 Mambo ya Nyakati 4:18-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Sulemani alitengeneza vyombo hivyo vyote kwa wingi sana; uzito wa shaba haukujulikana.+
19 Sulemani alivitengeneza vitu vyote+ vya nyumba ya Mungu wa kweli: madhabahu ya dhahabu;+ meza+ na mikate ya wonyesho iliyokuwa juu ya meza hizo;+ 20 vinara vya taa na taa zake za dhahabu safi,+ ili ziwake mbele ya chumba cha ndani zaidi kulingana na maagizo; 21 na maua, taa, na koleo, vyote vya dhahabu, dhahabu safi kabisa; 22 mikasi ya kukatia tambi za taa, mabakuli, vikombe, na vyetezo, vyote vya dhahabu safi; na lango la nyumba, na milango ya ndani ya Patakatifu Zaidi,+ na milango ya nyumba ya hekalu, ya dhahabu.+
-