-
2 Mambo ya Nyakati 5:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kwa hiyo mabawa ya makerubi yalikuwa yamenyooshwa juu ya mahali ambapo Sanduku liliwekwa, hivi kwamba makerubi hao walilifunika Sanduku na fito zake.+ 9 Fito hizo zilikuwa ndefu sana hivi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Patakatifu mbele ya chumba cha ndani zaidi, lakini hazikuonekana kutoka upande wa nje. Nazo ziko huko mpaka leo hii. 10 Hakukuwa na kitu kingine ndani ya Sanduku hilo isipokuwa yale mabamba mawili ambayo Musa aliyaweka humo kule Horebu,+ Yehova alipofanya agano+ na Waisraeli walipokuwa wakitoka Misri.+
-