-
2 Mambo ya Nyakati 6:3-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kisha mfalme akageuka na kuanza kulibariki kutaniko lote la Waisraeli huku kutaniko lote la Waisraeli likiwa limesimama.+ 4 Akasema: “Na asifiwe Yehova Mungu wa Israeli, ambaye kwa kinywa chake mwenyewe alimwahidi baba yangu Daudi, na kwa mkono wake mwenyewe ametimiza, akisema, 5 ‘Kuanzia siku niliyowatoa watu wangu nchini Misri, sijachagua jiji katika makabila yote ya Israeli na kujenga humo nyumba ili jina langu likae humo,+ nami sijamchagua mwanamume atakayekuwa kiongozi wa watu wangu Waisraeli. 6 Lakini nimechagua Yerusalemu+ ili jina langu likae humo, nami nimemchagua Daudi awatawale watu wangu Waisraeli.’+ 7 Na moyo wa Daudi baba yangu ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 8 Lakini Yehova akamwambia Daudi baba yangu, ‘Moyo wako ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, na ulifanya vizuri kutamani jambo hilo moyoni mwako. 9 Hata hivyo, hutajenga nyumba hiyo, lakini mwana wako mwenyewe utakayemzaa* ndiye atakayeijenga nyumba hiyo kwa ajili ya jina langu.’+ 10 Yehova ametimiza ahadi hiyo aliyoitoa, kwa maana nimechukua mahali pa baba yangu Daudi na kuketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli,+ kama Yehova alivyoahidi.+ Pia nimejenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli, 11 na humo nimeliweka Sanduku lenye agano+ ambalo Yehova alifanya na Waisraeli.”
-