10Ndipo Samweli akachukua chupa ya mafuta na kuyamimina juu ya kichwa cha Sauli.+ Akambusu na kusema: “Yehova amekutia mafuta uwe kiongozi+ juu ya urithi wake.+
24 Samweli akawaambia watu wote: “Je, mnamwona yule ambaye Yehova amemchagua,+ kwamba hakuna yeyote aliye kama yeye kati ya watu wote?” Basi watu wote wakaanza kupiga kelele wakisema: “Mfalme na aishi muda mrefu!”
10 Sasa Absalomu akawatuma wapelelezi katika makabila yote ya Israeli, akawaambia: “Mara tu mtakaposikia sauti ya pembe, tangazeni hivi: ‘Absalomu amekuwa mfalme katika Hebroni!’”+
12 Kisha Yehoyada akamtoa nje mwana wa mfalme+ na kumvika taji na Ushahidi,*+ wakamweka kuwa mfalme na kumtia mafuta. Wakaanza kupiga makofi na kusema: “Mfalme na aishi muda mrefu!”+