-
2 Mambo ya Nyakati 14:11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Kisha Asa akamlilia Yehova Mungu wake+ akisema: “Ee Yehova, haijalishi kwako ikiwa wale unaowasaidia ni wengi au hawana nguvu.+ Tusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea* wewe,+ na katika jina lako tumekuja kupigana na umati huu.+ Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu. Usiache mwanadamu anayeweza kufa akushinde.”+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 20:5, 6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Ndipo Yehoshafati akasimama katika kutaniko la Yuda na Yerusalemu ndani ya nyumba ya Yehova mbele ya ule ua mpya, 6 akasema:
“Ee Yehova Mungu wa mababu zetu, je, wewe si Mungu mbinguni;+ je, huna mamlaka juu ya falme zote za mataifa?+ Mkononi mwako mna nguvu na uwezo, na hakuna anayeweza kushindana nawe.+
-