Zaburi 51:5 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 5 Tazama! Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa,Na mama yangu alinichukua mimba katika dhambi.*+ Zaburi 130:3 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 3 Ikiwa ungekuwa unatazama* tu makosa, Ee Yah,*Basi ni nani, Ee Yehova, angeweza kusimama?+ Mhubiri 7:20 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 20 Kwa maana hakuna mtu mwadilifu duniani anayefanya mema sikuzote na hatendi dhambi kamwe.+ Waroma 3:23 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 23 Kwa maana wote wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,+ 1 Yohana 1:8 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 8 Ikiwa tunasema, “Hatuna dhambi,” tunajipotosha wenyewe+ na kweli haimo ndani yetu.