-
2 Mambo ya Nyakati 8:7-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Na watu wote waliobaki, yaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi+ ambao hawakuwa sehemu ya Waisraeli,+ 8 wazao wao waliobaki nchini—wale ambao Waisraeli hawakuwaangamiza+—Sulemani aliwaandikisha ili wafanye kazi ya kulazimishwa mpaka leo hii.+ 9 Lakini Sulemani hakumfanya Mwisraeli yeyote kuwa mtumwa wake,+ kwa sababu walikuwa mashujaa wake, wakuu wa makamanda wake wasaidizi, na wakuu wa waendeshaji wa magari yake ya vita na wapanda farasi wake.+ 10 Kulikuwa na wakuu 250 wa wasaidizi wa Mfalme Sulemani, waliokuwa wasimamizi wa watu.+
-