-
1 Wafalme 9:20-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Watu wengine wote waliobaki miongoni mwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ ambao hawakuwa sehemu ya taifa la Israeli,+ 21 wazao wao waliobaki nchini, ambao Waisraeli walishindwa kuwaangamiza, Sulemani aliwaandikisha ili wafanye kazi ya kulazimishwa kama watumwa mpaka leo hii.+ 22 Lakini Sulemani hakumfanya Mwisraeli yeyote kuwa mtumwa,+ kwa sababu walikuwa mashujaa wake, watumishi, wakuu, makamanda wasaidizi, wakuu wa wale walioendesha magari yake ya vita na wapanda farasi wake. 23 Kulikuwa na wakuu 550 wa wasaidizi waliosimamia kazi ya Sulemani, wasimamizi wa watu waliokuwa wakifanya kazi.+
-