-
2 Mambo ya Nyakati 9:3-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Sulemani,+ nyumba aliyojenga,+ 4 chakula kilichokuwa mezani pake,+ jinsi watumishi wake walivyoketi, jinsi watumishi wake walivyohudumu mezani na pia mavazi yao, na wale waliompa vinywaji na jinsi walivyovalia, na dhabihu zake za kuteketezwa alizotoa kwa ukawaida katika nyumba ya Yehova,+ alipigwa na bumbuazi.* 5 Basi akamwambia mfalme: “Habari nilizosikia katika nchi yangu kuhusu mafanikio* yako na kuhusu hekima yako zilikuwa za kweli. 6 Lakini sikuamini habari hizo mpaka nilipokuja na kujionea kwa macho yangu mwenyewe.+ Na kwa kweli sikuwa nimeambiwa hata nusu ya hekima yako nyingi.+ Umezidi kwa mbali habari nilizosikia.+ 7 Wenye furaha ni watu wako, na wenye furaha ni watumishi wako wanaosimama mbele yako daima, wakiisikiliza hekima yako! 8 Na asifiwe Yehova Mungu wako, ambaye amependezwa nawe, akakuweka kwenye kiti chake cha ufalme ukiwa mfalme kwa niaba ya Yehova Mungu wako. Kwa sababu Mungu wako anawapenda Waisraeli,+ na ili kuwafanya wadumu milele, alikuweka kuwa mfalme juu yao ili utekeleze haki na uadilifu.”
-