Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 10:4-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Sulemani,+ nyumba aliyojenga,+ 5 chakula kilichokuwa mezani pake,+ jinsi watumishi wake walivyoketi, jinsi watumishi wake walivyohudumu mezani na pia mavazi yao, na wale waliompa vinywaji, na dhabihu zake za kuteketezwa alizotoa kwa ukawaida katika nyumba ya Yehova, alipigwa na bumbuazi.* 6 Basi akamwambia mfalme: “Habari nilizosikia katika nchi yangu kuhusu mafanikio* yako na kuhusu hekima yako zilikuwa za kweli. 7 Lakini sikuamini habari hizo mpaka nilipokuja na kujionea kwa macho yangu mwenyewe. Na kwa kweli sikuwa nimeambiwa hata nusu yake. Hekima yako na ufanisi wako umezidi kwa mbali habari nilizosikia. 8 Wenye furaha ni watu wako, na wenye furaha ni watumishi wako wanaosimama mbele yako daima, wakiisikiliza hekima yako!+ 9 Na asifiwe Yehova Mungu wako,+ ambaye amependezwa nawe, akakuweka kwenye kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wa milele wa Yehova kwa Waisraeli, alikuweka rasmi kuwa mfalme ili utekeleze haki na uadilifu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki