15 Basi mfalme hakuwasikiliza watu, kwa sababu Yehova ndiye aliyesababisha badiliko hilo la mambo,+ ili atimize neno ambalo Yehova alimwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya+ Mshilo.
2 Kwa hiyo Yeroboamu akamwambia mke wake: “Tafadhali, inuka, badili sura yako ili watu wasitambue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu, halafu uende Shilo. Tazama! Nabii Ahiya yuko huko. Yeye ndiye aliyesema kwamba mimi nitakuwa mfalme wa watu hawa.+
29 Na mambo mengine katika historia ya Sulemani,+ kuanzia mwanzo mpaka mwisho, je, hayajaandikwa katika maandishi ya nabii Nathani,+ katika unabii wa Ahiya+ Mshilo, na katika kumbukumbu ya maono ya mwonaji Ido+ kumhusu Yeroboamu+ mwana wa Nebati?