-
2 Mambo ya Nyakati 10:12-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Yeroboamu na watu wote wakaja kwa Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyokuwa amesema: “Rudini kwangu siku ya tatu.”+ 13 Lakini mfalme akawajibu kwa ukali. Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akakataa ushauri wa wanaume wazee. 14 Akawajibu kama alivyoshauriwa na vijana wa rika lake, na kusema: “Nitafanya nira yenu iwe nzito zaidi, nami nitazidisha uzito wake. Baba yangu aliwaadhibu kwa mijeledi, lakini mimi nitawaadhibu kwa mijeledi yenye miiba.” 15 Basi mfalme hakuwasikiliza watu, kwa sababu Mungu wa kweli ndiye aliyesababisha badiliko hilo la mambo,+ ili atimize neno ambalo Yehova alimwambia Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshilo.+
-