-
2 Mambo ya Nyakati 11:1-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Rehoboamu alipofika Yerusalemu, mara moja aliikusanya nyumba ya Yuda na kabila la Benjamini,+ mashujaa 180,000 waliozoezwa,* ili wapigane na Waisraeli na kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu.+ 2 Kisha neno hili la Yehova likamjia Shemaya+ mtu wa Mungu wa kweli: 3 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani mfalme wa Yuda na Waisraeli wote walio Yuda na Benjamini, 4 ‘Hivi ndivyo Yehova anavyosema: “Msipande kwenda kupigana na ndugu zenu. Kila mmoja wenu arudi nyumbani kwake, kwa maana nimesababisha mambo haya yatukie.”’”+ Basi wakalitii neno la Yehova na kurudi, nao hawakwenda kupigana na Yeroboamu.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 25:5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Na Amazia akawakusanya pamoja watu wa Yuda na kuwaagiza wasimame kulingana na koo zao,* chini ya wakuu wa maelfu na chini ya wakuu wa mamia kwa ajili ya watu wote wa Yuda na Benjamini.+ Akawaandikisha waliokuwa na umri wa miaka 20 na zaidi,+ akapata kwamba walikuwa mashujaa 300,000 waliozoezwa* kwa ajili ya utumishi wa kijeshi, walioweza kutumia mkuki na ngao kubwa.
-