Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 11:1-4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Rehoboamu alipofika Yerusalemu, mara moja aliikusanya nyumba ya Yuda na kabila la Benjamini,+ mashujaa 180,000 waliozoezwa,* ili wapigane na Waisraeli na kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu.+ 2 Kisha neno hili la Yehova likamjia Shemaya+ mtu wa Mungu wa kweli: 3 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani mfalme wa Yuda na Waisraeli wote walio Yuda na Benjamini,⁠ 4 ‘Hivi ndivyo Yehova anavyosema: “Msipande kwenda kupigana na ndugu zenu. Kila mmoja wenu arudi nyumbani kwake, kwa maana nimesababisha mambo haya yatukie.”’”+ Basi wakalitii neno la Yehova na kurudi, nao hawakwenda kupigana na Yeroboamu.

  • 2 Mambo ya Nyakati 25:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Na Amazia akawakusanya pamoja watu wa Yuda na kuwaagiza wasimame kulingana na koo zao,* chini ya wakuu wa maelfu na chini ya wakuu wa mamia kwa ajili ya watu wote wa Yuda na Benjamini.+ Akawaandikisha waliokuwa na umri wa miaka 20 na zaidi,+ akapata kwamba walikuwa mashujaa 300,000 waliozoezwa* kwa ajili ya utumishi wa kijeshi, walioweza kutumia mkuki na ngao kubwa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki