-
1 Wafalme 12:21-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Rehoboamu alipofika Yerusalemu, mara moja aliikusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benjamini, mashujaa 180,000 waliozoezwa,* ili wapigane na nyumba ya Israeli na kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Sulemani.+ 22 Kisha neno hili la Mungu wa kweli likamjia Shemaya+ mtu wa Mungu wa kweli: 23 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani mfalme wa Yuda na nyumba yote ya Yuda na Benjamini na watu wengine, 24 ‘Hivi ndivyo Yehova anavyosema: “Msipande kwenda kupigana na ndugu zenu Waisraeli. Kila mmoja wenu anapaswa kurudi nyumbani kwake, kwa maana nimesababisha mambo haya yatukie.”’”+ Basi wakalitii neno la Yehova na kurudi nyumbani, kama Yehova alivyowaambia.
-